Thursday, July 22, 2010

VUVUZELA IMEANZA ENZI ZIPI?



Historia inasemaje?


Kumekuwa na maswali mengi kuhusu asili au chanzo cha vuvuzela , chombo kilichotumika kama sehemu ya burudani hivi karibuni huko bondeni. Je! unajua chimbuko lake au hawa wanasingiziwa tu? kama itakuwa kweli unajifunza nini ?
Je! hii inakamilisha usemi usemao "USILOLIJUA NI KAMA USIKU WA GIZA"

Tuesday, July 13, 2010

Ngoma zetu.

Historia inaonesha babu na bibi zetu walikuwa na utamaduni asilia, lakini kizazi cha leo kimebebwa na mitindo ya utamaduni wa kigeni. Bila shaka maamuzi ya kizazi kipya kama miziki yao inavyojitambulisha yalikuwa sahihi kutokana na sabubu walizoziona wao.

Ukiangalia kipande hiki cha ngoma asilia ijulikanayo kama "acrobatic snake dance" utaona radha tofauti na ubora wa tamaduni za wahenga wetu. Ngoma au utamaduni wetu wa asili ulikuwa unatukumbusha mambo mengi ya kijamii, kisiasa, kiuchumi, kiimani na hata kutuelimisha kisaikolojia. Utamaduni wa kigeni kutoka "ughaibuni" una radha tofauti na isiyokidhi hali halisia ya mazingira yetu tulolisishwa na babu zetu.


Utandawazi unatuweka sote kama kijiji kimoja lakini swali lakujiuliza ni kuangushwa kwa utamaduni wetu wa kiafrika na kujikuta tunakuwa na utandawazi ulojaa sura moja ya vionjo vya kiutamaduni.
Mimi nafikiri tuige mfano wa kaa (au crab) anayejongea kwa kwenda mbele na nyuma pia. Tusisahau tutokako japo kuna umhimu wa kutazama tuendako. Mtu huenda akawa si jasiri sana kama hajiamini au hawezi kujivunia hata kile kidogo alichonacho. MUNGU KATUJALIA MAMBO MENGI WAAFRIKA TUJIAMINI NA TUULINDE UTAMADUNI WETU.

Monday, July 12, 2010

Karibuni ndugu!

Nawakaribisha kwenye kibaraza hiki, nikiwa mgeni kidogo, natambua umuhimu wa kubadilishana mawazo kuelimisha na kuburudisha kuwa ndio msingi mkubwa wa IT. Kwa kiasi nategemea uwepo wenu mtandaoni uwe na msaada kwa wanaoanza na sio kuwa na mtazamo wa kujuana. Karibuni sana