Wednesday, September 15, 2010

Life after college

Mara nyingi maisha baada ya chuo huwa magumu kwa baadhi ya wahitimu. Hili tatizo huja pale mhitimu anapokuwa amejipangia malengo yake ya kimaisha lakini mwajiri wake hugeuka kuwa mbogo mahali pa kazi.

Kumekuwa na manyanyaso mengi katika vituo vingi kwa watumishi pale wakuu wa vituo wanapowabana wahitimu wengi kukosa nafasi za kuhudhuria semina mbalimbali za watumishi, kuishi ndani ya kituo bila kupata nafasi ya kwenda nje ya kituo. Wasiwasi wa wakuu wengi kuogopa kuporwa madaraka yao na watumishi katika vituo vyao waliojiendeleza limekuwa tatizo mojawapo linalofanya waishi kwa shida.
Wahitimu wengi kutoka vyuo vikuu hujikuta hawatimizi malengo yao na mazingira ya kazi kuzidi kuwa magumu kwao. Swali linabaki kwa hawa wakuu wa vituo vya taasisi mbalimbali kuwa kwa nini wasitumie muda wao kujiendeleza kielimu badala ya kuendelea kugombana na watumishi?