Sunday, December 19, 2010

MKONGWE WA FARISAFA.

Nawasalimuni wote ndugu zangu. Naomba nirejee tena na mada hii ambayo imenipa kufikiri sana bila kupata muafaka wa mawazo yangu. Nimejihisi kuwa labda nimekuwa mvivu wa kusoma maandiko matakatifu ya Mungu.
Yesu anatajwa sana habari zake na hivi karibuni tunaelekea kusherehekea sikukuu ya kuzaliwa kwake. Pamoja na jitihada zote za kutaka kufahamu kwa nini Yesu alikuwa na uwezo mkubwa sana wa kujibu maswali yote aliyoulizwa, nimekosa habari zake muhimu.
  • Yesu mnazareti, aliyezaliwa na Bikira Mariam, alisoma shule gani na chuo kipi?
  • Naomba kujua kiwango chake cha elimu.
Makuhani, Maliwali, Mafarisayo na wasomi wengine waliuliza maswali mengi kutaka kumtega, lakini Yesu alikuwa na uwezo wa kutoa hadi "reference" kwa kusema " IMEANDIKWA". Hata nyoka alipotaka kumjaribu Yesu, alijibu "IMEANDIKWA usimjaribu Bwana Mungu wako"
  • Kwa nini walimwita Mwalimu hata wasomi waliokuwa na elimu ya juu katika Uyahudi?

"NAWATAKIA CHISTMAS NJEMA NA HERI YA MWAKA MPYA 2011"

Friday, December 17, 2010

BIDHAA FEKI

Mfumo wa elimu Tanzania umejikita zaidi katika masomo ya nadharia kuliko vitendo. hali hii imetuathiri sana wananchi kwa sababu wengi wetu hatuna ubunifu wa kutosha wa kumudu ushindani wa soko la leo duniani. Ukipita mtaani utajionea bidhaa nyingi zijulikanazo kwa jina la 'MCHINA' zikiwa zimesambaa kila kona. Ukitafuta uwiano na kile tunachozalisha sisi dhahili utagundua tofauti kubwa.
Bidhaa za kigeni.

Viwanda vyetu viko wapi hadi tumevamiwa na bidhaa toka ughaibuni na kuziba vya kwetu?. Tusaidieni enyi watanzania mlioko nchini China, Japani, Korea, India kama huko mitaani kuna bidhaa zetu za kitanzania zinazouzwa zikiwa na nembo ya TBS na chata ya MADE IN TANZANIA.
Kaulimbiu ya nchi inasema 'KILIMO KWANZA' lakini ukienda shopright utakutana na bidhaa kama apple, coffee, milk, juice, onions, na matunda mengi kutoka nchi za nje kama Afrika kusini, kwa nini tusijivunie na vya kwetu? hii kaulimbiu ni ya majukwaani tu?
 
Haya nayo lazima yatoke nje?
Nafikiri ni vyema zaidi kama sera za uzalishaji mali na ukuaji wa viwanda za nchi zingetoa kipau mbele katika kukuza soko la bidhaa zetu asilia. Hata kama zitaonekana kuwa sio bora kama za wenzetu hapo ndipo tutajua jinsi ya kurekebisha na kukidhi mahitaji ya ushindani katika masoko yetu na ya nje.