Sunday, December 19, 2010

MKONGWE WA FARISAFA.

Nawasalimuni wote ndugu zangu. Naomba nirejee tena na mada hii ambayo imenipa kufikiri sana bila kupata muafaka wa mawazo yangu. Nimejihisi kuwa labda nimekuwa mvivu wa kusoma maandiko matakatifu ya Mungu.
Yesu anatajwa sana habari zake na hivi karibuni tunaelekea kusherehekea sikukuu ya kuzaliwa kwake. Pamoja na jitihada zote za kutaka kufahamu kwa nini Yesu alikuwa na uwezo mkubwa sana wa kujibu maswali yote aliyoulizwa, nimekosa habari zake muhimu.
  • Yesu mnazareti, aliyezaliwa na Bikira Mariam, alisoma shule gani na chuo kipi?
  • Naomba kujua kiwango chake cha elimu.
Makuhani, Maliwali, Mafarisayo na wasomi wengine waliuliza maswali mengi kutaka kumtega, lakini Yesu alikuwa na uwezo wa kutoa hadi "reference" kwa kusema " IMEANDIKWA". Hata nyoka alipotaka kumjaribu Yesu, alijibu "IMEANDIKWA usimjaribu Bwana Mungu wako"
  • Kwa nini walimwita Mwalimu hata wasomi waliokuwa na elimu ya juu katika Uyahudi?

"NAWATAKIA CHISTMAS NJEMA NA HERI YA MWAKA MPYA 2011"