Sunday, June 5, 2016

MAHUSIANO

_1.Ule usemi kuwa wanaume wa Dar wanakula chips mayai badala ya ugali wa dona kuwa ni chanzo cha migogoro ktk mahusiano kwa wapenzi wao HUENDA IKAWA SIO KWELI kwa kuzingatia kanuni za lishe bora ni ipi..... _2.Uzuri wa sura,rangi au umbo eti ni kipaumbele katika mahusiano......pia sio kweli kwa mujibu wa uzoefu... Nionavyo mimi Wazo zuri la ugali wa dona,lakini sizani kama ugali ndio tatizo pekee,maana hata ughaibuni hawali dona na mahusiano yao yako Juu. Lishe ni mhimu lakini haisababishi mahusiano yawe bora pasipokujua virutubisho vya mahusiano. *Illiterate* wa mahusiano anaweza kuwa mme au mke, ugal hatukatai bali ifahamike hiyo siyo mechi ya _simba na yanga_ ni zaidi ya kutumika kwa *energy* kama tafsiri ya ugali ilivyo. Partners can be all *energetic enough* for the marathon yet can not achieve the satisfaction point " *climax*" . partners used to ignore _sex education_ , pretending to know more than what the truth counts. Mfumo rasmi wa Elimu hauna somo la mahusiano,ni jukumu la mhitaji kutafuta ujuzi na maarifa nje ya mfumo rasmi. Bahati mbaya wasomi wengi ni waathirika wa mambo haya sababu wanajiona wanajua kumbe hawajui. Mapenzi hayana cha _prof,Dr wala kilaza_, na ni bora kujifanya huyajui ili utafute kujua. *SATISFACTION* ?? Swali linakuwa _how do I satisfy him/her_ ? _how do I know that he/she is sexually satisfied_ ? _does satisfaction refers to bed sex alone_? _do partners knows all about intimacy_? Sumu ya mahusiano ni jambo la kufahamu pia. Wapendanao waachane na *kiburi,ubabe,ukatili,dharau,ujuaji usio na tija,utapeli,usaliti,uongo,udanganyifu,ulaghai,aibu,woga,uchafu,umaskini,uvivu,uzembe, tafsiri potoshaji za kidini n.k* siwezi taja yote mengine yanategemea matakwa ya wapendanao _e.g sigara,ulevi,wizi,ujambazi,ushirkina,uchawi,uporaji,ugomvi,n.k_ haya yanategemeana na wapendanao. 2. Ikumbukwe uzuri wa sura,rangi au umbo la mwanamme/mwanamke ni sehemu ndogo sana katika suala zima la utosherevu wa kimahusiano, ni vigezo vidogo sana kati ya vingi vingine. Laiti ingekuwa hivyo bilashaka warembo walioko baa ( *bar-made* ) wangekuwa wameolewa sababu wanasifa zote kwa mwonekano wa nje, WANAMVUTO WA SURA NA SHEPU.... Wengi wameharibu mahusiano yao kwa kuwalinganisha wapenzi wao na wale wa kwenye mitandao ya kijamii,au kutaka wapenzi wao wafanye au kuiga kama yaonekanayo ktk mitandao. Sidhani kama ni vizuri kutaka mwenzi aonekane au kufanana na kila sifa ya uzuri ionekanayo ktk mitandao, Mungu hakutuumba wote sawa kwa sura,rangi wala maumbo. Hata hivyo hayo yananafasi Ndogo sana ktk mahusiano. Tusisahau, hakuna mbabe wa mapenzi. Ni bahari pana na kila mtu anaogelea kwa kadri awezavyo kupiga mbizi. Tujifunze tusiridhike na elimu ndogo ya mahusiano tuliyonayo. Tujitahidi kuyajua mahusiano kwa mapana yake. 👩‍❤️‍👩. 👫. 💃🏃🏻 Mungu atuwezeshe kujua yale tusiyoyajua. Mimi sio mtaalamu sana niache uwanja wazi wengine watasema zaidi.

No comments: