Sunday, October 31, 2010

RAISI MPYA TZ.

Ni siku nzuri ambayo watanzania tunatimiza haki yetu ya kikatiba na bado masaa machache sasa tufikie hatima ya kuwa na raisi mpya. Nimeamka alfajiri na mapema kuwahi kituoni. Niwapongeze wananchi kwa moyo wa kutekeleza haki yenu na ninaamini mwamko huu utasaidia sana kufikia malengo mazuri.
Baadhi ya vituo vimeripotiwa kuwa na kasoro ndogondogo na kwa ujumla hali ni shwari katika vituo vingi. Tutulize mawazo tusubili majibu ya kura zetu.
Unauwezo wa kutabili nani atakuwa RAISI wako masaa machache yajoyo? BONYEZA HAPA

Saturday, October 30, 2010

UANACHAMA BILA KUPIGA KURA.


Watanzania tuwe na moyo wa kupenda kutumia nafasi yetu kumpigia kura kiongozi ambaye atatuletea mafanikio kwa kujali na kusikiliza mahitaji ya wananchi. Tusikae nyumbani siku ya kupiga kura tukitegemea kuwakilishwa na wenzetu. Uzarendo wetu kama watanzania uonekane kesho katika vituo vya  kupigia kura.
Tukumbuke kuombea nchi yetu tupate kiongozi BORA NA MWADILIFU, nawapa pole sana wanafunzi wa vyuo vikuu ambao mmeshindwa kufanikisha zoezi la kufika katika vituo vyenu vya kupigia kura. Tumieni nafasi hii kuwatakia kila la heri wale waliofika katika vituo vyao kutimiza haki yao ya kikatiba.

Monday, October 11, 2010

KIDATO CHA NNE 2010.

Nawapa hongera wote kwa kumaliza kidato cha nne. Jiandaeni na maisha ya mtaani. A-Level Schools are very few in Tanzania, get prepared to face life challenges.

You had long journey of four years, but that is just the begining, CONGRATULATIONS