Tuesday, July 13, 2010

Ngoma zetu.

Historia inaonesha babu na bibi zetu walikuwa na utamaduni asilia, lakini kizazi cha leo kimebebwa na mitindo ya utamaduni wa kigeni. Bila shaka maamuzi ya kizazi kipya kama miziki yao inavyojitambulisha yalikuwa sahihi kutokana na sabubu walizoziona wao.

Ukiangalia kipande hiki cha ngoma asilia ijulikanayo kama "acrobatic snake dance" utaona radha tofauti na ubora wa tamaduni za wahenga wetu. Ngoma au utamaduni wetu wa asili ulikuwa unatukumbusha mambo mengi ya kijamii, kisiasa, kiuchumi, kiimani na hata kutuelimisha kisaikolojia. Utamaduni wa kigeni kutoka "ughaibuni" una radha tofauti na isiyokidhi hali halisia ya mazingira yetu tulolisishwa na babu zetu.


Utandawazi unatuweka sote kama kijiji kimoja lakini swali lakujiuliza ni kuangushwa kwa utamaduni wetu wa kiafrika na kujikuta tunakuwa na utandawazi ulojaa sura moja ya vionjo vya kiutamaduni.
Mimi nafikiri tuige mfano wa kaa (au crab) anayejongea kwa kwenda mbele na nyuma pia. Tusisahau tutokako japo kuna umhimu wa kutazama tuendako. Mtu huenda akawa si jasiri sana kama hajiamini au hawezi kujivunia hata kile kidogo alichonacho. MUNGU KATUJALIA MAMBO MENGI WAAFRIKA TUJIAMINI NA TUULINDE UTAMADUNI WETU.